Jipongeze Ulipoweza, Jihoji Uliposhindwa Mwezi Huu Juni

Habari mfuatiliaji wa blogu hii kila siku, leo ni tarehe 30 ya mwezi huu wa sita. Kuna jambo la shukrani kwa Mungu kukuwezesha katika siku za awali na hata sasa ukingo wa mwezi huu. Nikupongeze kwa juhudi yako ya kujifunza kila siku katika blogu hii. Utakua umepiga hatua kubwa kama mwezi huu ulijitoa kwa kufanya …

HUWEZI JIDANGANYA MWENYEWE

Habari Mfuatiliaji wa Blogu hii kila siku, leo ni siku ya pekee haijawahi kuishiwa na mtu zaidi yako, kumshukuru Mungu ni wimbo wako wa kwanza uwe kuwa pumzi na afya uliyonayo ni ya kuitumia vizuri kwa ajili ya kujiboresha na pia kuishi vyema na wengine. Leo ni fursa nyingine ya kuweza kufanya unayosema nitafanya, fursa …

MAMBO 11 NILIYOJIFUNZA MWEZI JUNI NA SIKU CHACHE KUELEKEA KWISHA

Habari mfuatiliaji wa blogu hii kila siku, ni wakati mwingine wa tafakari ya kuelekea mwishoni mwa mwezi wa sita, kama ulivyokua umeanza na sasa ukingo umeshafika wa mwezi huu kuishia, tukipata nafasi ya pumzi ni mlango wa mwezi wa saba kuingia, kuna mengi yakujifunza katika mwezi huu yalikuwepo, na kama uliweza kuwa na muda kufikiri …

USILEGEZE KAMBA KWA USHINDI MDOGO

Habari mfuatiliaji wa blogu hii kila siku.leo ni siku njema kabisa, pumzi na nguvu ni fursa tumeipata neno la shukrani ni la muhimu sana kwa Mungu, maana mambo yote yapo katika muda na pumzi, hivyo pumzi hii si ya kudharau na kuipa thamani ndogo. Ni fursa kubwa sana ya kuendelea na mipango na kuwa na …

THROUGH THE PATIENT’S EYES

MAMBO 15 NILIYOJIFUNZA KATIKA KITABU CHA THROUGH THE PATIENT’S EYES ( Kupitia Macho Ya Mgonjwa ) Eneo la afya ni eneo linalomgusa kila mmoja kama si kuumwa basi kulazwa na kama si kulazwa basi ni kumhudumia ndugu, mzazi au mtoto akiwa hospitalini, kina maelezo ya kina juu ya huduma za afya kwa mgonjwa akiwa hospitalini …

Kuona bado Kama tuna Muda Mwingi

Habari mfuatiliaji wa blogu hii kila siku, hii ni siku nyingine kama ni kalenda basi ni tarehe nyingine tena, Shukrani kwa Mungu uwe ni wimbo wako kila siku kuwa hata kufika hapa ni neema na zaidi kuipa heshima siku ya leo kwa kuitumia vizuri na kuendelea na juhudi katika malengo yako na ndoto yako. Muda …

Kila Kitu kilianzia Chini, Usilaumu kipindi cha Ukuaji

Habari mfuatiliaji wa blogu hii kila siku tunayo kila sababu ya kumshukuru Mungu kuona siku mpya tena, hii itupe kuwa na vinywa visivyokauka shukrani kwa kuona siku mpya, hii ni siku ya pekee hakuna aliyewahi kuiishi hivyo ni muhimu kuipa heshima kwa kuutunza kwanza muda na pili kwa kujitahidi kufanya yale yanayotusogeza katika mipango yetu …

Usiruhusu Kauli “Bora Liende

Habari mfuatiliaji wa blogu hii kila siku, ni siku nyingine tena zinazidi kusogea na muda unaenda kila siku hakuna namna ya kuurudisha nyuma, hivyo kamwe mida hauwezi kuchelewa labda itokee kujichelewesha tu kwa mipango na malengo yetu, ni jambo la kumshukuru Mungu kuwa Maisha ni Pumzi, na pumzi hii si ya bora liende au ngoja …

Design a site like this with WordPress.com
Get started