518; January 18, RUDI KUWA WEWE

Habari Rafiki ni siku nyingine tena ya kuangalia maisha yetu yalipo na wapi tuendako. Siku kama hii ni fursa kubwa ya kuchukua hatua na kuanza vitu tukiwa na nguvu bado lakini tukiwa na nafasi ya kuwa hai. Maisha yetu yanaisha kila siku na inakuwa hatari sana pale yanapoisha na tukiangalia nyuma hakuna hatua kubwa ambazo …

517; January 17, SOTE TUNA VIBANZI SHUGHULIKA NA CHA KWAKO

Rejea ya Maarifa; Hoja za Karugendo, Gazeti Mwananchi Na. 6739 Ukurasa wa 18. Habari ya siku mpya Rafiki ni leo ambayo kwa wakati wa jana ulisema ikifika basi utaanza au kuchukua hatua. Kila siku ni nafasi ya wazi ili tujiboreshe na tuongezeke kifikra ili tuweze kukua na kupata maendeleo. Hakuna maendeleo katika fikra ambazo zinakwepa …

516; January 16, Nyuma ya pazia ndipo penye siri sio ukionacho sasa

Habari Rafiki siku inapoisha huwa ni jambo gani kwako unalikumbuka ?. Kama unakumbuka ni jinsi gani siku yako ulivyoipoteza pasipo kufanya jambo lenye kugusa maisha basi jionee huruma sana na ujiadhibu kabisa kwanini unapoteza sehemu ya maisha yako. Kila siku ni kama tunakufa kidogo kidogo kabla ya kifo halisi siku kuwa kati kati yetu. Je …

515; January 15, Kusikiliza hupelekea kuwa na hekima

Habari Rafiki kila siku katika maisha yetu huja kama zawadi na wenye kuifungua ni sisi wenyewe kwa maana ya kujimimina katika vilivyo ndani yetu ( ujuzi, uzoefu, kipaji, maono, mawazo ) katika kusaidia wengine wapige hatua. Maisha yako yakikosa kugusa maisha ya watu wengi basi kuna kiwango chako cha ndani hujakitumia ipasavyo na muhimu kujiona …

514; January 14, Fedha itakufuata ukishaweka mazingira ya yenyewe kuja kwako

Maisha ni kanuni na kadri unavyokwepa kanuni za maisha kuna mambo ambayo ulitakiwa upate kirahisi utalazimika kuingia gharama kubwa zaidi na gharama hiyo ni upotevu wa muda na nguvu. Kuna matokeo bora sana kila wasaa ambao utakuwa unafuata kanuni hasa kanuni za maisha ambazo zimekuwa zinatoa majibu sawa na vile watumiavyo wengine. Fedha ni eneo …

513; January 13, Mambo hayakai yakadumu hufika wakati hupita.

Habari Rafiki ambaye huachi kujifunza kila siku ukijua wazi kuwa bila kujifunza hakuna ukuaji na ukikosekana ukuaji hakuna maendeleo. Hongera kwa hii hatua nzuri ambayo unajisukuma kupiga hatua zaidi ya ulipokuwa jana. Karibu katika kujifunza tena katika yale ambayo yanatutokea, tunayaona na yalikwisha kutokea. Unapokuwa katika wakati mgumu au wakati wenye wingi wa changamoto utaona …

512;January 12, Itachukua muda vuta Subira

Maisha na asili ni walimu walio wazuri katika kuishi kwetu siku zote hapa Duniani. Masomo mapana na ya kina yapo katika haya maeneo mawili ya kuishi kwetu maisha na asili. Kuna mengi ambayo yamefichwa ndani ya maisha na ndani ya asili yasoweza kuwa rahisi kupatikanika kwa watu ambao wanachelea kujifunza. Asili inatufundisha juu ya kungoja …

511; January 11, Ushindi mkubwa ni kuzishinda hisia na kutawala mawazo yako

Habari Rafiki kila siku ni siku ambayo inatupa nafasi ya kujifunza maisha kwa kina ikiwa tutakuwa tayari kujifunza. Tukikosa tu kujifunza basi tunakaribisha maisha ambayo hayafai kuishiwa. Safari ya kujifunza ina faida nyingi kuliko hasara za kutojifunza. Kujifunza kila siku ni kujiweka kuwa imara na maisha yako yanakuwa bora kila siku zaidi ya siku ya …

510; January 10~PIGO MOJA la NYUNDO HALITOSHI KUPASUA MWAMBA

Maisha ya wadudu yanaweza kutupa somo kubwa sana na moja ya somo kubwa la hekima ni katika hawa wadudu wawili ambao nimekuwa najifunza mengi ikiwa ni kwa zaidi ya miaka 20 sasa ni juu ya uendelevu wa kila siku na hatua ndogo ndogo zao kufanya mambo makubwa. Ukimtazama mchwa utaona jinsi ukubwa wa vichuguu vyao …

509; January 09, Zawadi pekee ya kujipa ukiwa peke yako ni kufikiri juu ya maisha yako

Maisha yetu yanaweza kuwa bora sana endapo tutajipa wasaa wa kuyaangalia kwa kina maisha yetu na wapi tulipokuwa mwanzo, tulipo na kule tuendako. Tafakari ya kina kama hii ni wasaa wa maisha bora sana ambayo si wote wanaweza kupata. Jinsi ambavyo ratiba na mambo mengi yamewabana sana wasiweze kufikiri juu ya maisha kunazidi kuwa na …

Design a site like this with WordPress.com
Get started