Kuishi unachokisema ni kazi ngumu. Ila izoe hivyo hivyo.

Je ungoje kuweza kuishi unachokisema kabla ya kusema ?. Je useme kisha uende kuchukua hatua kuishi ulichokisema?. Ni maswali magumu ambayo unaweza kujiuliza wewe au watu wengine kuwauliza wanaoandika au kusema kitu kwa wengine. Kuishi ni zoezi gumu na linataka uanze kuwa muwazi kwako mwenyewe kabla ya watu wengine kuwa tayari kukuona u muwazi. Ni …

NIFUNZE KUWA MUUZAJI

Marko Kinyafu Muumini wa kweli, +255 (0) 714 129 520 Kinyafumarcos@gmail.com Kitunda, Dar es salaam, Tanzania Dr.Raymond Mgeni Malenga wa Ubena, +255 (0) 676 559 211 Raymondpoet@yahoo.com Mbeya, Tanzania Kinyafu Marko; Mwalimu wangu mwalimu, naanza nayo dawia Leo nimetia timu, hapa kwako kukujia Ninalo jambo muhimu, nataka kulitambua Ati miye nifanyaje, niwe muuzaji bora? Dr.Raymond …

Umezaliwa ili uisaidie Dunia kuwa bora

Mwaka 2018 nilipata fursa ya pekee ya kusoma kitabu cha “The ASSIGNMENT” kilichoandikwa na Mike Mudrock. Kitabu hiki nilipewa zawadi na ndugu yangu mmoja ambaye tulionana katika duka la vitabu “HOUSE OF WISDOM” maeneo ya Posta. Huyu ndugu alikuwa akinitafuta na wakati mwingine tunatafutana ili anipe hiyo zawadi ambayo hadi leo hii nabaki kuona kama …

Kuwa na fikra za utele na fikiri kitajiri.

Fikra za utele zinakufanya uone maisha yana wingi wa vitu kuliko vile ambavyo una fikra za uhaba. Unapoweka fikra zako katika kuwa na kitu ndivyo shauku kubwa ya kuumbika kwa hicho kitu hutokea. Hili liko wazi sababu mawazo ni nguvu na ni nguvu ambayo wakati wote hujitafuta ijitokeze katika umbo. Unaweza kuona hili halina nguvu …

Hujachelewa kuanza kusoma vitabu.

Habari rafiki yangu. Naamini unaendelea vizuri na hatua zako za kila siku. Nafasi uliyonayo sasa kuwa hai ni zawadi ya pekee sana. Itumie kujiboresha kila inapoitwa leo bila kukata tamaa. Kuna wakati utajaribu utaanguka ila usife moyo kuendelea kujaribu na kujiboresha wewe kila siku. Jua kuwa hakuna kitu kinakuwa bora kwa siku moja bila majaribio …

647; Ukiona mtu yupo mbali ujue alipotoka ni mbali.

Leo hebu tulia na vuta picha ya kila mtu unayejifunza kitu kutoka kwake na ona nyuma ya pazia kabla ya huyo mtu kufanikiwa alipitia changamoto zipi. Ukiangalia kwa kina utaona safari ya yeye kuwa hapo alipofika ilichukua muda mrefu kufika hapo. Unaweza kuvutika na mtu alivyoweza kuwa na utajiri na kujenga jina kubwa kibiashara au …

646; Kuna njia nyingi za kufanya kitu chochote. Jisukume kufikiri zaidi ya unavyofikiri

Kama leo utasema uende mkoa mmoja hadi mwingine unaweza kutumia njia nyingi za usafiri. Unaweza kutumia usafiri wa anga, barabarani na majini. Hata usafiri wa barabarani unaweza kutembea kwa miguu, baiskeli, pikipiki au gari. Kinachotofautisha ni gharama ambayo utaingia katika kutumia njia za usafiri kufika eneo lingine. Ila njia za kufanya kitu bado zinaendelea kuwa …

Design a site like this with WordPress.com
Get started