Ninatazama Mlima – “Natakiwa nipande na kufika juu kileleni”

Kughairisha ni mlima, uvivu ni mlima, kutothubutu ni mlima. Mlima una vikwazo na kufika juu ya mlima basi lazima upande na kutoruhusu vikwazo vikufanye usifike juu kileleni. Maisha yetu ni mikusanyiko ya vilima mbalimbali ambavyo bila kuwa tayari au kuwa watu jasiri hatuwezi kupata ushindi wowote mkubwa maishani. Kughairisha ni kikwazo kikubwa sana ambacho kinatuchelewesha …

Mwonekano unaweza kukudanganya- “Kisogelee hicho kitu karibu”

Mwonekano wa vitu na bila kufikiri kwa kina umefanya tuingie katika matatizo mengi ambayo yangeepukika endapo tungejipa muda wa kukisogelea hicho kitu kwa karibu. Inawezekana mtu ukavutika na mwonekano wa kitu na ulipokisogelea na kuona kumbe mwonekano ulikuwa ni juu juu tu na si vile kilivyo ulivyokiona. Jambo moja kubwa ni mafanikio ya jambo lolote …

Ukomavu wa juu wa maisha- “Kujisimamia bila kusukumwa”

Maisha tulonayo sasa ni matokeo ya karibu asimilia 80 za yale tunayoyafanya kuliko tunayoyaongea. Hili ndilo linatupa maisha tulonayo sasa na kutoka hapa tulipo ni kuamua kufanya kwa utofauti kuliko tulivyokuwa tunaendelea kufanya. Maisha ni wajibu wetu bila kuwa na mtu wa kutusukuma sukuma tufanye tunayopaswa kufanya. Ngazi ya Wewe mwenyewe kuweza kujisimamia bila msukumo …

Ukipenda unachokifanya kitakufikisha mbali- “Upendo una NGUVU”

Wanasema katika maisha kuna nguvu kubwa mbili zinazoyaongoza maisha yetu. Mosi ni nguvu ya “HOFU” na pili ni nguvu ya “UPENDO”. Watu wanafanya vitu katika msukumo wa hizi nguvu ukiangalia kwa kina. Mtu asipoongozwa na upendo basi hofu itachukua nafasi ya kumwongoza. Nguvu ya hofu inawadidimiza watu kupata vitu vingi bora maishani na watu wanajawa …

Unapoitazama siku kama siku ya mwisho- “Leo imejitosheleza”

Kuna mambo mengi tunayaghairisha katika maisha yetu hili tunalifanya kwa kuona huenda bado muda tunao. Ila tumekuwa mashahidi kwa kuona namna wengi ambao tulokuwa nao miaka 5 ilopita hawapo sasa. Hili linatukumbusha namna ambavyo kila siku tuwapo na nafasi ya uzima ni mwaliko wa kuitumia siku hiyo kama ni siku ya mwisho na hatuna nafasi …

Safari ya maisha itakupitisha katika mengi- “Jifunze kukaza moyo”

Ukweli wa maisha ni kuwa tutaendelea kupitia changamoto siku zote za maisha yetu. Utakaposema kuwa umemaliza changamoto moja basi itatokea nyingine. Hata kufanikiwa nako hakuachi kutokuwa na changamoto sawa sawa na mafanikio apatayo mtu. Kujua kweli hii inakusaidia kuwa mtu imara na kukubali uhalisia wa maisha ni uwepo wa kuvuka vihunzi vya changamoto kila siku …

Tunakua kupitia vile visivyotupa furaha au matokeo sasa – “Maumivu hutukomaza”

Maumivu ya msuli baada ya zoezi kufanyika ndio mwanzo wa kuimarika kwa misuli ya mtu. Kuumia kimwili pale unapofanya hatua ya kuamka mapema kila siku ndivyo unavyojipa nafasi ya kukomaa kitabia kwa kuendelea kuamka asubuhi na mapema bila shida. Mwanzo wa jambo hasa yaliyo na matokeo mazuri baadaye huwa yafanyikapo sasa hayatupi furaha bali huwa …

Asili ina funzo la uendelevu- “Kuchomoza na kuzama kwa Jua”

Asili ni utele wa mambo yote tuonayo na pengine wakati mwingine tusoyaona au kuyashika ila yapo mfano hewa, upepo, sauti, mwanga na kadhalika.  Asili inatupa picha nzima ya kuendelea kwa vitu na hili linaonekana pale ambapo tunajifunza maisha ya mbegu ilivyo. Mbegu yoyote ile imebeba nguvu ya uzao ndani yake. Tunaona namna mbegu moja ya …

Unachokirudia kinakupa kukitawala au kitakutawala.

Fundi mzoefu anapata sifa moja kubwa ya kuitawala kazi yake na humpa watu wengi wamfahamu kwa ustadi wake au ufundi wake. Unapochunguza kwa kina unakuja kuona ufundi wake unatokana na marudio marudio ya kukifanya kitu kwa muda mrefu. Kiasili ni hali ya kawaida kuwa kile unachokirudia muda mrefu unakipatia uzoefu na kukibobea na wakati huo …

Wakati wa sasa ni mtaji wa kuanza kufanya kitu- “Ijayo haitabiriki”

Sijui kama Dunia ilikuwa inajua kama mwaka 2020 ungekuwa mwaka wa tofauti kwa matukio yenye kutikisa Dunia kama mlipuko wa “CORONA” ungebadili mambo mengi na kuathiri hata mifumo ya kibiashara kimataifa. Yote ni angalizo la namna maisha yetu wakati pekee mzuri wa kujiandaa au kuanza kufanya kitu ni sasa. Wakati unaofikiri baadaye utafanya huenda usipate …

Design a site like this with WordPress.com
Get started