ANZA 7; Kazana Kila Kila Siku, Unapoenda Licha Ni Mbali ila Ni Karibu.

Kuendelea kufanya kitu kila siku sio kazi ndogo katika maisha yetu ya kila siku. Siku huwa hazifanani, kuna siku unaamka huna morali ya kufanya kitu na zipo siku ambazo unaamka una morali au hamasa ya kufanya kazi. Hivyo si jambo linaloweza kuwa jepesi kuwa kila siku uendelee kuwa na morali ile ile kama siku za …

ANZA 6; Mtaji ni Watu, Kuza Mtandao wa Watu Kila Siku

Kufikia mwaka 2030 basi kuna jambo moja kubwa la muhimu litakalokuwa na soko kubwa zaidi kutokana na nafasi ya kukua kwa mawasiliano. Jambo hili kubwa ni sanaaau ujuzi ya kuhusiana na watu “Networking art”. Watu wanaofaidika na chochote kile wanachokifanya wamekwisha jua au tambua thamani ya mtaji watu “social capital”. Kupitia watu ndipo unapopata chochote …

ANZA 5; Usikate Tamaa, Ukikata Tamaa Walio Nyuma Yako Watakwama.

Unajua ni kwa namna gani ndoto ya mtu mmoja inaposhindwa kutimizwa si inamnyima mtu fursa ya kuifikia bali inawakwamisha maelfu ya watu ambao huenda maisha yao yangekuwa bora kwa mtu mmoja kuweza kutimiza maono au ndoto yake. Mtu anapokata tamaa kuendelea na kile alichokianzisha anafunga njia kwa maelfu ya watu nyuma yake. Kukata tamaa ni …

ANZA 4; Endelea Kutafuta Majibu ya Matatizo Yanayoisumbua Jamii

Jamii tunayoishi ina bahari ya matatizo ambayo kamwe hayawezi kuisha. Mafanikio yanapojitokeza basi na matatizo yanakuja kwa namna nyingine. Hivyo ukiweka nguvu hili eneo la kutafuta majibu juu ya matatizo yanayoisumbua jamii basi unaweza kuwa na mchango mkubwa kwa maisha ya watu, ukafanikiwa na kuisaidia jamii kupiga hatua. Magunduzi yote ambayo tunayaona ni watu waliokuja …

ANZA 3; Anza Kutafuta Maarifa yahusuyo Unachokifanya

Hatua ya kuanzisha kitu ni ngumu ila inaweza kuwa nyepesi pale ambapo unaanza kuwa na mwanga kuhusu hicho kitu. Mwanga au nuru ya kitu haiji tu ghafla ila isipokuwa kuamka kimaarifa na kiufahamu. Ndo maana lipo himizo la utafute maarifa, ufanye tafiti na uulize walokutangulia ili upate hatua za kwenda. Watu wengi wameingia katika kushindwa, …

ANZA 2; Mwanzoni ni Pagumu Ila Usighairishe Ulichokianzisha

Safari ya chochote unachokianza ambacho hukuwahi kuanza ni lazima utakutana na kikwazo au changamoto kwa kukiona kigumu mwanzoni. Hili lipo kwa kuanzisha tabia mpya, kuacha tabia fulani, kujenga nidhamu fulani au kuanzisha mfumo fulani mpya. Akili zetu zinapenda mazoea yaliyo ya faraja “Comfort zones”. Sasa kinachotokea unapoanzisha kitu kipya ni kulazimisha akili itoke katika hali …

ANZA 1; Anzia Ulipo na Utarekebisha Mambo Mbele ya Safari

Tumejichelewesha sana kuanzisha vitu kwa kutafuta tuwe na kila kitu. Hili limefanya wengine hadi wafe na mawazo yao kwa kusema nitaanza nikiwa na hiki na hiki. Nani aliye na uhakika wa kuwa kesho itakuwa yake tena ?. Anza hapo hapo ulipo na kadri muda unavyoenda utajua wapi pa kurekebisha. Kungoja uwe na kila kitu utajichelewesha …

Unapenda Kusoma Vitabu?, twende Pamoja 2021.

Kila mwaka huwa ninaandaa orodha ya vitabu navyosoma mwaka unaoanza ingawa huwa naanza mwaka wangu mpya kila ifikapo mwezi wa 11 wa kila mwaka. Hili nimekuwa nafanya sasa kwa miaka mitatu baada ya kujifunza mengi kupitia Kisima cha Maarifa, kundi ambalo lipo chini ya usimamizi wa Kocha Dkt. Makirita Amani. Toka nimeanza kufanya hivyo imekuwa …

Design a site like this with WordPress.com
Get started