614: Huu ndio ufunguo ambao kila mmoja anao wa kuweza kutumia kufanikiwa.

Habari Rafiki. Karibu katika mwendelezo wa safari ya maarifa kila siku za maisha yetu. Maarifa ni mwanga na ndio njia ya mkato ukitaka kufanikiwa na kufanya makubwa. Najua wewe nawe kwa namna moja utakuwa umewahi kuona namna baadhi ya watu wakivuta utajiri, mafanikio, nguvu na mambo yote bora katika maisha kama wanafanya hayo yatokee kwa …

613: Njia 10 za kuboresha mfumo wa kuongeza wateja katika biashara yako.

Habari Rafiki. Naamini unaendelea na hatua zako kila siku za kusogea hatua moja zaidi. Biashara ndio njia moja inayoweza kukusaidia kuelekea utajiri. Biashara ndio mfumo unaoweza kukusaidia kuendelea kutengeneza thamani kwa kutatua matatizo na kukidhi mahitaji ya jamii husika. Biashara kuendelea lazima iwe na wateja. Wateja unaweza kufananisha na damu ilivyo mwilini. Biashara ili ikue …

612: Mei 12, Asili ni mama na vile mama alivyo na upekee wake ndivyo asili ilivyo linganifu na Mama.

Mama hubeba uzao na uzao ndio kiini cha maisha ya kizazi kimoja na kingine. Mama hubeba zawadi ya maono, mawazo, ubunifu na biashara zinazozaliwa na uzao ambao hubeba katika ustahimilivu. Furaha na uzalishaji na mwendelezo wa maisha huambatana na sifa hii. Asili hutusitiri na kubeba rasimali zote kwa ajili ya uendelevu wa maisha, kila kitu …

611: Mei 11, Endelea kujisukuma ili uweze kuona matokeo unayotamani kupata.

Kuna wakati utaamka na kuona siku kama imekuwa na changamoto hata kabla siku kuanza. Wakati huu wengine husema siku ishakuwa mbaya au imeingiwa mkosi. Ni kweli mwili huchoka na unakuwa ukikupa kila sababu ya wewe kuacha kujisukuma kama mwanzo na kujikuta hakuna kitu unachopiga hatua. Hakuna njia ya mkato ambayo utapita kama utakwepa kujisukuma mwenyewe …

610: Mei 09, Mtu wa ndani anavyopambana kuliko mtu wa nje.

Maisha huanza kuwa na uhuru pale ambapo utafika hatua ya kudhibiti mtu aliyeko ndani yako. Mtu aliye ndani ndiye amebeba uhalisia wa mtu mzima. Kinacholeta shida si kilicho nje bali ni kile kilicho ndani. Hisia, mawazo yote husababisha matokeo ya nje ya mtu. Ukosefu wa udhibiti wa mtu wa ndani ndipo penye msingi mbovu wa …

609: Mei 07, Ni muhimu kujua wakati wako ili usije kuona kama uko nyuma unapojilinganisha na wengine

Siku hii moja ina watu wa rika mbalimbali. Wapo walio katika nafasi ya utoto, ujana, utu uzima na uzee. Kila mmoja yu katika wakati wake. Si eneo hili pekee hutokea hivi wazi wazi pia yapo maeneo mengine yenye kufanana na haya. Kila mmoja hupita wakati wake katika kujifunza, kujizoesha na kupata kujua mambo kwa kina …

608: Mei 06: Kuni zinateketea, ongeza nyingine moto uendelee kuwaka.

Ukiwa jikoni kuna ile hali inayovutia sana ya moto wa kuni unavyokuwa unakolea kila unapokuwa unaongeza kuni. Moto kuwaka kunaleta mwanga na kama ni chakula basi kina uhakika wa kupata joto lenye uhakika wa kuivisha kilicho juu ya moto. Vitendo vyako ni kuni ambazo zinachochea moto wako ( shauku, ndoto, lengo, kipaji nk ) ili …

607: April 26, Kila unapotaka kuacha ulichokianzisha kumbuka sababu ya kukianza.

Ni rahisi katika maisha kuanzisha vitu vingi na kumaliza hadi mwisho wanaomaliza hubakia wachache. Kuanza ni kama vile unavyokuwa na hamasa siku ya kwanza ya kitu. Lakini kadri siku zinavyokwenda unajikuta hamasa haina nguvu tena bali kinachobakia ni nidhamu pekee yake. Maisha yanataka uwe na nidhamu ya kumaliza ambacho umekianza. Ushindi na pongezi ni vile …

606: April 24, Swali la kitu unalojiuliza ndilo jibu ukiangalia kwa kina.

Katika safari ya maisha si jambo geni unapofikia wakati ambao unakuwa na maswali mengi juu ya vitu, hali na watu. Unaweza ukawa unajiuliza nifanye nini kuwa na furaha, nifanye nini niwe mtu bora au nifanye nini nipate kuona njia. Ukiangalia haya maswali kwa kina yana majibu kwa kila swali. Kuwa na furaha, kuwa bora na …

605: April 23, Siku ya Vitabu Duniani na zawadi moja kubwa unayoweza kuipata pekee kwa kuvisoma vitabu.

Leo ni siku ilowekwa Duniani kote kwa kuhimiza suala la usomaji na usomaji vitabu ikiwa ni jambo la kwanza, uchapishaji na masuala ya hati miliki za kazi za uandishi. Huenda isiwe siku kubwa kama siku nyingine ambazo huhamasishwa na kukumbukwa Duniani kote. Ila kwa aliye msomaji wa vitabu au chanzo chochote cha maarifa basi siku …

Design a site like this with WordPress.com
Get started