Tembea Maeneo tofauti tofauti ili Ujifunze Mambo Mapya.

Ufanyikaji wa biashara wa eneo moja na lingine hufanywa tofauti na kama ni mfanyabiashara anayetembea maeneo tofauti tofauti anapata vitu vipya na vitu vipya vinasaidia kukuza biashara yake. Kutembea eneo mbali na unapofanya kazi yako au shughuli za kujitafutia riziki kunapanua kuona mambo au kujifunza njia mpya ya kuendesha biashara au uuzaji wa bidhaa au …

Mtiririko [Flow] Unapojitokeza Ndani Yako Usiuzimishe, Bali Upe Njia.

Safari yangu ya uandishi na ushairi nimekutana na hali ambazo awali nilishangaa sana maana sikupata kuzielewa. Hizi hali ni pale ambapo kujikuta napata msukumo usiokauka wa kuandika au kutunga mashairi bila kuchoka na wakati huo nikiwa napitia hali nzuri ndani yangu nisoweza kuelezea. Hizi hali zimekuwa zinajitokeza mara kwa mara na nilijipa ahadi kuwa zikiendelea …

Unahitaji utulivu ili uchukue hatua bora

Mwaka 2017 ilikuwa mara yangu ya kwanza kufahamu falsafa na falsafa ambayo nimetokea kuipenda na kuendelea kujifunza kila siku ni falsafa ya Ustoa. Moja ya jambo kubwa nilovutiwa na falsafa hii ni juu ya kumsaidia mtu kujenga utulivu wa ndani. Utulivu wa ndani kama ikifananishwa na bidhaa sokoni basi ni bidhaa adimu sana katika zama …

Upendo ni Nguvu, Kazi bora ni matokeo ya upendo.

Kama ilivyo chuki au hofu zilivyo na nguvu kubwa maishani ndivyo upendo ulivyo na nguvu kubwa katika maisha yetu ya kila siku. Katika maisha tunaongozwa na hizi nguvu kubwa mbili; Hofu na upendo. Ingawa asimilia kubwa hofu imekuwa inaongoza kuliko upendo. Upendo una nguvu kubwa ya kuumba kitu chenye ubora kuliko hofu. Ubora wa kazi …

Rafiki wako wa kweli wa mafanikio – “Soma vitabu sasa”

Wakati naanza vitabu nikiwa bado kijana mdogo sikuweza kuona nguvu yake. Ila kadri muda ulivyoenda ndivyo nilivyoanza kuona vitabu ni rafiki wa kweli wa Maisha ya mafanikio. Kila nilipopitia changamoto nyingi katika maisha, vitabu vimekuwa njia kubwa ya kujifunza, kuona mwanga na kunisaidia kuvuka vikwazo. Rafiki wa kweli huyu amekuwa ni rafiki wa faida karibu …

Kila hatua unayochukua ina mchango kule unakotaka kufika

Hatua ndogo ndogo tunazoendelea kuchukua katika maisha yetu zina mchango mkubwa wa matokeo ambayo tunayapata maishani. Matokeo yoyote makubwa ni matokeo ya mkusanyiko wa hatua ndogo ndogo, machaguzi au maamuzi ya mambo anayofanya mtu kila siku. Usijekudharau hatua yoyote ile iwe kwa udogo au kwa ukubwa ukidhani haina mchango wowote kule unakotaka kufika. Kinachotuchelewesha kufanikiwa …

Kila kinachokutokea kinakuimarisha – “Mambo hutokea yatakavyo”

Naheshimu kila siku nayopata ya kuona, kutembea, kujifunza na kujiboresha nikiwa naamini haya ni mambo muhimu kwa mtu anayeheshimu zawadi ya maisha. Maisha yanatusaidie tuone, tutembee, tujiboreshe, tujifunze na katika hayo yote tupate kukua. Ukuaji wetu wa fikara na hisia ni ukuaji muhimu katika kumsaidia mtu awe mtu mkomavu. Ingawa mambo haya ni mazuri ila …

Jitolee kwanza kabla hujapata fursa unayoitaka

Kujitolea kunaeleweka pengine tofauti tofauti na watu mbalimbali. Wengine wanaona kujitolea ni kudidimizwa na kutumiwa bila faida na wengine wanaona kujitolea ni msingi na ngazi ya kwanza kuweka mguu kupanda kule wanakotamani kufika. Leo tugusie eneo la pili namna kujitolea kulivyo na manufaa kabla hujapata kile ulichokuwa unakitafuta maishani. Ujuzi na uzoefu ni mahitaji makubwa …

Kazi zote bora hutokeaje tokeaje ?

Utakuwa umewahi kupitia hali fulani ya kuzipongeza kazi zote za zamani kuwa zilikuwa bora kuliko sasa utakuta kuna msemo uitwao "Old is Gold" kwa maana ya "kale ni dhahabu". Huenda hicho kitu ni muziki fulani umesikia basi unasema ama kweli watu wa zamani walifaidi sana. Nyimbo, picha, maisha ya kale, watu mashuhuri wa zamani utaona …

Safari ya Maisha ni ya pekee na Kila mtu hupitia mambo kwa majira yake – “Kila Mtu na Wakati wake”

Si kweli wakati ambao unapitia magumu wewe basi ndivyo kwa kila mtu wakati huo anapitia magumu. Wakati ambao wengine wanalia au kupitia changamoto za maisha wengine wanaendelea kufurahia maisha na kufanikiwa zaidi. Hili ni funzo kubwa la maisha kuwa kila mtu ana safari ya pekee na hupaswi kuidharau safari yako kwa kujilinganisha na watu wengine. …

Design a site like this with WordPress.com
Get started