Unaumia kihisia kwa matarajio unayodhania- Uhalisia mambo ni TOFAUTI

Agosti 04- Jua mambo yanaweza kuwa tofauti na unavyodhania Mwezi huu nipo nasafiri katika uwanda wa ngazi nne za uwepo. Ngazi ya hisia, mwili, kiroho na kiakili ikiwa ndio safari kamilifu maishani ya kutembea yenye kuzalisha maisha imara na bora. Unaweza kuwa imara kimwili lakini ukikosa uimara wa hisia, kiroho na kiakili bado unakuwa mtu …

Litapita kama mengine yalivyopita- ni SOMO la USTAHIMILIVU

Agosti 3- Mambo hayana makao ya kudumu maishani. Hili nalo litapita tu kama mengine yalivyopita Maisha ni darasa linalotufunda mengi kila iitwapo leo. Darasa hili lina kila aina ya mitihani na mafunzo kama si mambo yanayokutokea Wewe basi kuna watu unawaona wanapitia mitihani na mafunzo mengi. Licha ya hayo yote yanayotokea kuna muda mambo hupita …

Juhudi ni Rafiki wa Kweli [ 1 N ]

“All growth depends upon activity. There is no development physically or intellectually without effort, and effort means work.” – Calvin Coolidge Ukuaji wowote ule unategemea KAZI. Hakuna maendeleo ya kimwili au kiakili bila juhudi. Juhudi kwa maana ya kazi fulani inahitajika kufanyika. Maneno hayo juu yana nguvu kubwa kwangu napokumbuka mengi kuhusu maisha yangu. Juhudi ndio …

Mwezi Agosti – Kitabu cha kusoma [The Four Levels of Healing by Shakti Gawain ]- Ngazi nne za Uponyaji – Mtu ni ngazi nne za Uwepo

-Imarisha ngazi zote nne maisha yawe KAMILI Binadamu ni uwepo wa mambo makubwa manne; Kiroho, kiakili, kihisia na kimwili. Huu mkusanyiko kwa pamoja ndio unaofanya utimilifu na utoshelevu maishani. Haya maeneo manne ni ya kuendelezwa, kuponywa na kufanywa yawe pamoja ili maisha yaitwayo ya maana yaweze kutokea. Ngazi hizi nne ndizo zinazofanya tuone maisha ya …

Bisha hodi nao mlango utafunguliwa- Safari ya Utambuzi

Hodi!,Hodi!, Hodi!  [Tumezoea kubisha hivyo katika milango majumbani mwetu ila ni muda hatujabisha hodi ndani yetu kujua kilichomo ] – Agosti 1 2020 Kama tungeweza kufungua hazina zilizopo ndani yetu kamwe tusingeweza kupata eneo lingetosha kuzibeba. Hii ni dhahiri namna ndani ya kila mmoja wetu kuna hazina na utajiri ambao mtu akikuza nafasi ya kutambua …

Miaka 10 ijayo nitakuwa mbali kama nitaamua kuweka kazi kubwa sasa ! – UTAYARI ndio Ada

Kuweka kazi ni kuweka nguvu, akili, muda katika kufanya lengo ulojiwekea ulifikie. Kuweka kazi ni kuwa tayari kukabiliana na kila aina ya changamoto na kusema changamoto hazitakuzuia kusonga mbele. Kuweka kazi kubwa ni kuhakikisha unajikana kabisa na kila aina ya mambo ambayo yatakuchelewesha kule unakotaka kufika. Miaka 10 kuanzia sasa kama nitaweka kazi kubwa katika …

Chagua kimoja na izamishe akili hapo.

Kila siku naiona ni zawadi nayopewa kuishi kitoshelevu. Uhai ni zawadi ya pekee mno nayoshukuru kwa Mungu kila iitwapo leo. Maisha yangu yanakuwa na maana sababu ya uwepo wa uhai. Hivyo kila siku nina kazi moja kubwa nayo ni kuizamisha akili katika jambo moja kila siku nalo ni UANDISHI. Uandishi ni njia moja ambayo naifurahia …

Alama za kudumu za kuiachia Dunia siku tutakapokufa.

Nikukaribishe tena katika safari ya kujifunza, kuishi na kufurahia zawadi ya kuwa hai. Uhai ni zawadi na inapaswa kutumika vizuri mno kila iitwapo leo. Pili ni furaha na utoshelevu wa pekee unapojua au kufanya kitu kinachokubeba moyo na akili zako zote kukifanya. Uandishi kwangu ni utoshelevu mkubwa ambao ninafurahia kila siku katika hii zawadi ya …

Mambo 28 nilojifunza mwezi Julai 2020

Habari rafiki yangu wa kipindi kirefu katika kufuatilia makala mbalimbali kupitia blogu hii toka mwaka 2017. Wewe umekuwa unanipa deni la mimi nisiache kuandika na nijisukume kukushirikisha mengi nayojifunza na kukutana nayo katika safari ya maisha yangu. Miaka 2 ilopita nilikuwa na utaratibu wa kuandika mambo ambayo kila mwezi nilokuwa najifunza. Lile zoezi lilikuwa bora …

Kila kitu kizuri kitakuhitaji uwekeze muda wa kutosha.

Mwezi huu wa saba nilijiwekea zoezi la kujifunza kila siku juu ya asili na nimefanikisha kwa sehemu kujua mengi kuhusu asili. Somo moja kubwa ambalo nimejifunza katika kipindi cha zaidi ya siku 20 za kujifunza asili nimekuja kugundua na kukumbushwa juu ya “Kila kitu kizuri kinahitaji uwekezaji muda wa kutosha”. Ni kauli nyepesi nyepesi kwa …

Design a site like this with WordPress.com
Get started